1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMyanmar

Utawala wa kijeshi wa Myanmar warefusha muda hali ya dharura

31 Julai 2023

Utawala wa kijeshi nchini Myanmar leo umetangaza kurefusha kipindi cha hali ya dharura kwa muda wa miezi sita zaidi, uamuzi unaotoa ishara ya kusogezwa mbele kwa tarehe ya uchaguzi uliahidiwa kufanyika mwezi Agosti.

https://p.dw.com/p/4Ubc7
Myanmar Militärputsch | Myint Swe, acting president
Picha: MRTV/Handout/REUTERS

Tangazo hilo limetolewa na Kaimu Rais Myint Swe mbele ya Baraza Tawala la Kijeshi ambapo amesema hali ya hatari iliyodumu kwa zaidi ya miaka miwili itarefushwa kwa kipindi kingine cha nusu mwaka kuanzia Agosti Mosi.

Soma zaidi: Myanamar: Jeshi limetangaza hali ya dharura na kuchukua madaraka
Jeshi la Myanmar lapinga cheo kipya cha Su Kyi

Sababu iliyotolewa ni kuendelea kwa mapigano kwenye mikoa kadhaa ya nchi hiyo na kwamba utawala wa kijeshi unahitaji muda zaidi kurejesha utulivu kabla ya kuondoa tangazo la hali ya dharura na kuitisha uchaguzi.

Myanmar imetumbukia kwenye mzozo mkubwa kisiasa tangu jeshi lilipompindua kiongozi wa kiraia, Aung San Suu Kyi, mwaka 2021 na kutekeleza hatua kadha za kukandamiza wakosoaji wake.