1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yasema ripoti ya IAEA haina mashiko

Amina Mjahid
27 Desemba 2023

Iran imesema hakuna chochote kipya katika ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kudhibiti nishati ya nyuklia IAEA, iliyosema Iran imeongeza uzalishaji wa madini ya urani baada ya miezi kadhaa kupunguza uzalishaji.

https://p.dw.com/p/4ad8X
Iran Teheran | Mkuu wa shirika la Atomiki la Iran Mohammad Eslami
Mkuu wa shirika la Atomiki la Iran Mohammad Eslami Picha: Atomic Energy Organization Of Ir/ZUMA/picture alliance

Mkuu wa shirika la Atomiki la Iran Mohammad Eslami amesema hakuna chochote kipya walichokifanya na shughuli zao zinafuata kanuni zilizopo, akiongeza kuwa wanaendelea kuzalisha asilimia 60 ya madini hayo na hakuna kilichoongezeka. 

Soma pia:Iran imeuonya Umoja wa Ulaya kwa kutaka kuiendelezea vikwazo ambavyo umoja huo iliiwekea kutokana na shughuli zake za nyuklia

Hopa jana IAEA ilitoa ripoti iliyodai Iran imezidisha kiwango chake cha uzalishaji wa madini hayo kwa kilo 9 zaidi tangu mwishoni mwa mwezi Novemba.    Urutubishwaji mkubwa zaidi wa madini ya Urani wa asilimia 90 ndio unaohitajika kutengeneza silaha za nyuklia.