1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Afrika Kusini yaishtaki Israel ICJ kwa 'mauaji ya kimbari'

Tatu Karema
30 Desemba 2023

Afrika Kusini imewasilisha kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) dhidi ya Israel kwa kile ilichokitaja kuwa vitendo vya "mauaji ya kimbari" katika ukanda wa Gaza

https://p.dw.com/p/4aih6
Kikao cha Kikao cha Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) mnamo Septemba 18, 2023
Kikao cha Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) Picha: International Court of Justice/UN Photo/Wiebe Kiestra

Kwa mujibu wa taarifa, kesi hiyo katika ICJ inahusiana na madai ya ukiukaji wa Israel wa jukumu lake chini ya Mkataba wa Mauaji ya Kimbari, na kusema kuwa "Israel imejihusisha, inajihusisha na inatishia kushiriki zaidi katika vitendo vya mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Palestina huko Gaza".

Soma pia:Wizara ya afya Gaza yasema vifo kutokana na vita na israel vimefikia 21,320

Katika kesi hiyo, Afrika Kusini pia inasema Israel imekuwa ikichukuwa hatua '' kwa lengo la kuwaangamiza Wapalestina katika Ukanda wa Gaza kama sehemu ya kundi pana la taifa, rangi na kabila la Palestina''.

Soma pia:Mkuu wa jeshi la Israel anasema vita dhidi ya Hamas vitaendelea kwa miezi mingi ijayo

Israel imepinga mashtaka hayo, huku msemaji wa wizara yake ya mambo ya nje Lior Haiat akiandika kwenye ukurasa wa X, ambao awali ulijulikana kama twitter kwamba  "Israel inakataa na kuchukizwa na kashfa inayoenezwa na Afrika Kusini na ombi lake''  kwa mahakama ya ICJ.