1. main content
  2. main navigation
  3. extra content
  4. head navigation
  5. search
  6. Choose form 30 Languages


 

 | 21.11.2009 | 04:00 UTC

Westerwelle akutana na Medvedev na Lavrov

MOSCOW

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ujerumani Guido Westerwelle amesema viongozi wapya waliochaguliwa kuuongoza Umoja wa Ulaya ni watu wenye uwezo na sasa wanakabiliwa na changamoto kubwa.

Kauli hiyo ameitoa mjini Moscow alipokutana na waziri mwenzake wa Urusi, Sergei Lavrov na Rais Dmitry Medvedev, katika ziara yake ya kwanza ya kikazi nchini Urusi. Akizungumza na waandishi habari, Westerwelle alisisitiza nia ya Ujerumani kuendeleza uhusiano mzuri uliopo baina yake na Urusi.

Naye Waziri Lavrov aliutaka Umoja wa Ulaya kuzungumza kwa sauti moja katika kutatua haraka masuala yanayoigusa dunia nzima. Aidha, viongozi hao walizungumzia pia mpango wa nyuklia wa Iran na suala la Afghanistan. Mwishoni mwa ziara yake ya siku moja, Westerwelle alikutana pia na wanaharakati wa kutetea haki za binaadamu nchini Urusi.



 
Picture of the Day
ImageOfTheDay

DW-TV EUROPE live

Journal - Nachrichten mit Tagesthema

We're sorry, due to legal issues this content can not be transmitted as live stream.

If you are inside the United States, it is still possible for you to enjoy DW-TV. For more information, please click here.

Wafanyakazi
Waliochutama kutoka kushoto: Sekione Kitojo,Halima Nyanza,Josephat Charo na Ramadhani Ali. Waliosimama kutoka Kushoto: Susanne Bergers-Rose,Abdul Mtullya,Saumu Mwasimba,Mohamed Abdulrahman,Othman Miraji, Andrea Schmidt,Thelma Mwadzaya, Mohamed Dahman,Oumilkher Hamidou,Samia Othman na Nina Markgraf

Kiswahili On Your Desktop via RSS
RSS