1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mazungumzo ya amani yatafana,yasema Ujerumani

Thelma Mwadzaya22 Agosti 2010

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amewatolea wito viongozi wa Israel na Palestina kushiriki kikamilifu katika mazungumzo mapya ya moja kwa moja yaliyo na azma ya kuisaka amani ya Mashariki ya Kati.

https://p.dw.com/p/OtN0
Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani Hillary Rodham Clinton akiitangza tarehe ya mazungumzo ya ana kwa ana ya Mashariki ya KatiPicha: AP

Bibi Merkel aliupongeza uamuzi huo wa kuyaanzisha upya mazungumzo hayo ya amani yaliyokwama mwaka 2008,pindi baada ya israel kuuvamia Ukanda wa Gaza.

Mazungumzo hayo yanatarajiwa kuanza rasmi ifikapo tarehe mbili mwezi wa Septemba ijapokuwa wanasiasa wa pande zote mbili husika wameshatoa tahadhari kuwa huenda kukatoea vikwazo.Kulingana na msuluhishi mkuu wa Palestina Saeb Erakat,upande wao utajiondoa kwenye vikao ikiwa Israel itaendelea na ujenzi wa makazi yake katika eneo wanalolikalia.Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon amesema kuwa mazungumzo hayo ni nafasi ambayo haipaswi kupotezwa.    

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Hillary Clinton alitangaza siku ya Ijumaa tarehe hiyo ya waIsrael na wapalestina kuanza mazungumzo ya moja kwa moja  kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miezi 20. Taarifa hizo ni kwa mujibu wa gazeti la Marekani la New York Times.

Israel Flash-Galerie Netanjahu ein Jahr im Amt Siedlungsbau
Mpalestina akifanya kazi ya ujenzi katika makazi ya Israel ya Shlomo yaliyo kwenye eneo la Jerusalem Mashariki.Picha: AP

Muda wa mwaka mmoja

Gazeti hilo limewanukuu  maafisa wawili ambao majina yao hayakutajwa, walioarifiwa juu ya hali hiyo, wakisema Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na  Rais wa Palestina Mahmud Abbas, wamekubaliana kuweka muda wa mazungumzo uwe mwaka mmoja.

Rais Barack Obama wa Marekani anatarajiwa kuwaalika Netanyahu na Abbas mjini Washington mapema mwezi ujao wa Septemba kuanza mazungumzo, yatakayo zingatia sehemu ya mwisho ya masuala tete ikiwa ni pamoja hatima ya  mji wa Jerusalem pamoja na kurejea kwa wakimbizi wakipalestina.

Kurejea katika mazungumzo, itakua ni hatua ya kwanza muhimu ya mafanikio kwa utawala wa Obama katika juhudi zake za kuyafufua mazungumzo ya amani ya Mashariki  ya kati.

Mazungumzo ya ana kwa ana baina ya Israel na Wapalestina yamekwama kwa karibu miaka miwili, licha ya shinikizo la Marekani kwa pande zote mbili.

Duru ya mwisho ya mazungumzo ya moja kwa moja ilivunjika , pale Israel ilipofanya hujuma ya wiki tatu ya kijeshi katika ukanda wa Gaza Desemba 2008 katika jaribio la kuzuwia mashambulio ya maroketi ayaliofanywa na wanaharakati wa  chama cha Hamas kinachotawala eneo hilo.

Wizara ya mambo ya nchi za nje ya Marekani imeonyesha kuwepo kwa matumaini juu ya  mazungumzo ya  ana kwa ana yanayopangwa kuanza mwanzoni mwa mwezi ujao.

Msemaji wa wizara hiyo Philip Crowley aliwaambia waandishi habari kwamba Waziri Clinton  ameshauriana na  Waziri wa mashauri ya kigeni wa Jordan Nasser Judah na  Waziri mkuu awa azamani wa Uingereza Tony Blair ambaye  ni mjumbe wa kundi la  pande nne zinazohusika na  suala la mashariki aya kati ambazo ni Marekani, Urusi, Umoja wa mataifa na Umoja wa Ulaya.

Barack Obama mit Benjamin Netanyahu und Mahmoud Abbas NO FLASH
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na Kiongozi wa Palestina Mahmoud AbbasPicha: AP

Ujenzi wa makazi una utata

Maafisa wa Palestiana wamesema hatua yoyote mpya  lizima iwe katika zingatio la  taarifa iliotolewa na  kundi  hilo la pande nne mjini Moscow na ambayo imeitaka Israel kusitisha ujenzi wa makaazi na hakikisho kwamba amazungumzo hayo yatafikia  mkataba wa mwisho katika kipindi cha miaka miwili. Lakini vyombo vya ahabari nchini Israel viliripoti wiki hii kwamba wajumbe saba katika baraza la mawaziri la Israel, waliikataa taarifa ya kundi hilo.

Israel ikashikilia iko tayari  kuingia  kwenye mazungumzo, lakini bila amasharti yoyote,

Netanyahu na Abbas waliizuru Washington mnamo miezi ya karibuni kwa mazungumzo tofauti na rais Obama, huku ikulu ya Marekani ikitoa wito kwa pande hizo mbili kuharakisha hatua ya  kuanza mazungumzo ya moja kwa moja.