1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MANU kileleni Premier league

27 Desemba 2010

Manchester United imekamata kiti cha uongozi wa ligi kuu ya Uingereza baada ya kuichapa Sunderland mabao 2-0.

https://p.dw.com/p/zqEY
Dimitar Berbatov aliyepachika mabao 2 katika ushindi wa Manchester UnitedPicha: picture alliance/dpa

Mabao yote ya MANU yaliwekwa wavuni na  Dimitar Berbatov. Katika mechi nyingine, Carlos Tevez aliliweka pembeni jinamizi la kutaka kuihama Manchester City, pale alipopachika mabao 2 kati ya 3 ambayo Manchester City iliichapa Newcastle United.

Tottenham Hotspur ikiwa nyumbani iliichapa Aston Villa mabao 2-1, huku Blackburn Rovers ikilambishwa mchanga nyumbani kwa kukandikwa mabao 2-0 na Stoke City.

Leo kuna kivumbi, pale Arsenal itakapopambana na mabingwa watetezi Chelsea.

Mwandishi:Aboubakary Liongo/Reuters

Mhariri:Josephat Charo